Burudani
Nick wa Pili aeleza kwanini wimbo wake mpya ‘Baba Swalehe’ umekuwa gumzo mapema
Rapper wa kundi la Weusi, Nick wa Pili amesema wimbo wake mpya ‘Baba Swalehe’ umekuwa gumzo mapema kutokana na ujumbe wake na jinsi alivyobadilika kwenye aina ya uchanaji.
Rapper huyo ameiambia Bongo5 kuwa wimbo huo utakuwa ni miongoni mwa nyimbo zake zitakazoishi kwa muda mrefu zaidi.
“Kichwa cha jina la wimbo kimechangia wimbo kwenda haraka, utofauti wa kilichoimbwa, ujumbe ni wa kufurahisha sana, muundo wa chorus ni mpya, beat hata michano ni vipya ndio kitu ambacho kimewagusa watu,” amesema Nick.
“Naona pia hii ni miongoni mwa nyimbo zangu ambazo zitaishi muda mrefu kama Sitaki Kazi. Kwahiyo Baba Swalehe ni kitu ambacho kitaendelea kupendwa na kuishi miaka mingi sana.”