![](https://bongo5.com/wp-content/uploads/2022/10/WhatsApp-Image-2022-10-27-at-11.35.28-AM.jpeg)
Mwimbaji Staa Ommy Dimpoz ameachia track list ya Album yake ambayo ataiachia rasmi siku ya ijumaa ikiwa ni album yake ya kwanza toka anze muziki
Album hiyo imepewa jina la Dedication na baada ya kupost official cover na list ya Ngoma ambazo amewashirikisha wasanii mbali mbali akiwemo Nandy, Marioo, Black Diamond, Fally Ipupa, Muda Keys na wengine. Aliambatanisha na caption inayosomeka
“LADIES & GENTLEMEN kwanza Napenda kuchukua nafasi hii Kumshukuru Mwenyezi Mungu Kwa Afya na Uzima Alhamdulilah 🙏🏽❤️pili kwa Furaha ya Kipekee Mwezi huu Tarehe 4 November 2022 siku ya Ijumaa panapo uzima Naenda kuandika historia mpya katika Maisha yangu kwani Album Yangu Ya kwanza toka nianze Muziki itatoka Rasmi jina la Album ni DEDICATION. Haikuwa Kazi Rahisi Ukizingatia Mapito niliyopitia Lakini kila kitu kina Muda wake.Shukrani za Dhati Kwa Watu Wote Ambao Wamesaidia mimi kufika hapa Kuanzia Team yangu,Familia,Marafiki na Wadau MbaliMbali Ambao kila mmoja ana mchango hata kama ni mdogo katika Maisha yangu kwa Ujumla Asanteni sana.” Ommy Dimpoz