Habari

Picha/Video: Femina yazindua kipindi kipya cha Fema TV show

Wakati tukielekea kwenye uchaguzi mkuu mwaka 2015, shirika la Femina Hip leo limetangaza kuanza kwa msimu mpya wa kipindi cha Fema TV.

Mtangazaji wa  Fema TV Show Rebeca Gyumi
Mtangazaji wa Fema TV Show, Rebeca Gyumi

Msimu huo umebeba jina la ‘Nguvu ya Binti’ ambao ni sehemu ya ajenda pana zaidi inayokwenda pia kwenye jarida la Fema ili kuhamasisha zaidi wasichana kujihusisha katika masuala ya uchaguzi.

Restless Development, Limmy Omary  wa Fema TV Show (kulia) akizungumza
Limmy Omary wa Fema TV Show (kulia) akizungumza kufafanua jambo mbele ya waandishi wa habari

Akizungumza na waandishi wa habari, mtangazaji wa kipindi hicho, Rebeca Gyumi alisema kipindi hicho kilicholenga kuelimisha wasichana kimeandaliwa kutoka kwenye mikoa mbalimbali ya Tanzania.

“Vipindi vitabeba ujumbe kwaajili ya wasichana wenyewe kuwahamasisha kushiriki michakato ya uchaguzi, kama haki na wajibu wao na kwamba wafanye hivyo kwa amani. Na uzalishaji wa kipindi umefanyika katika mikoa mbalimbali ya Tanzania ikiwemo Lindi, Njombe, Dodoma, Kigoma, Arusha na Dar es salaam,” alisema Rebeca.

Rebeca alisema kipindi hicho kitarushwa kwenye vituo vya runinga vya EATV na Star TV kila Jumapili na Jumatatu. Kipindi cha kwanza kitarushwa Jumapili hii, saa tatu kamili usiku kupitia EATV na Jumatatu, July 13 saa tatu na nusu usiku kupitia Star TV.

Alisema kama kawaida ya Fema Hip, burudani na elimu vitaenda sambamba na kwamba mfumo wa uwasilishaji wa kipindi umebadilika ili kuruhusu wadau zaidi kushiriki. Pia kwakuwa ni msimu mpya unaohusu nguvu ya binti, watangazaji ni mabinti wenye nguvu watakaokuwa zaidi ya watangazaji. Kutakuwepo na zawadi na vituko vya Bwana Ishi.

Team Nguvu binti wakiwa katika ubora wao
Team Nguvu ya binti wakiwa katika ubora wao

Waandishi wa habari wakichukua matukio
Waandishi wa habari wakichukua matukio
4K0A0698

4K0A0702

4K0A0706

4K0A0708

4K0A0709

4K0A0713

4K0A0721

4K0A0726

4K0A0741

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents