Habari

Rais Magufuli aweka wazi sababu za kumteua Mama Salma Kikwete

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli ameweka wazi sababu sababu ya kumchagua kuwa mbunge kwamba aliona atawawakilisha vizuri watu wa Lindi.

Rais Magufuli ameeleza sababu hizo Alhamisi hii wakati akizungumza wilayani Bagamoyo katika ziara yake ya siku tatu, mkoani Pwani.

“Nilimchangua mama Salma kikwete kwanza ana sifa nyingi, ya kwanza ni first lady mstaafu lakini pia yeye pia atawawakilisha vizuri watu wa Lindi lakini nilijua kwa upendo mkubwa alionao kwenye moyo wake ambapo alitoka kote Lindi njia zote hakuona mwanaume wakumuoa akaja hapa nikaona ana upendo mkubwa na nikaona nimpe ubunge kwahiyo ndugu zangu nina washukuru sana,”alisema Rais Magufuli.

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents