Burudani
Reekado Banks atoa jina la album yake mpya
Msanii kutoka nchini Nigeria aliye chini ya lebo ya Don Jazzy (Mavins Records), Reekado Banks kupitia post yake kwenye Instagram amewapa mashabiki jina la album yake mpya.
Album hiyo imepewa jina la SPOTLIGHT.
Jina halisi la Ricardo ni Ayoleyi Hanniel Solomon na mwaka 2014 alishinda Rookie of the Year kwenye tuzo za The Headies.