Rihanna atua nchini Senegal
Muimbaji wa muziki Rihanna ameungana na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kuboresha elimu katika mataifa yanayoendelea.
Wawili hao wamekutana nchini Senegal wiki hii katika mkutano wa Global Partnership for Education, mkusanyiko ambao ulihusisha rais wa Benki ya Dunia Jim Yong Kim na viongozi wa mataifa kadhaa ya Kiafrika.
kulingana na ABC News, Rihanna allienda nchini huko kwa niaba ya msingi wa Clara Lionel ambayo inafanya kazi katika mataifa maskini ya kutoa huduma za afya na programu za kielimu.
Today’s @GPforEducation Replenishment Conference in Dakar, Senegal raised over $2.3B for global education!📓✏️🌎 @rihanna @GlblCtzn #FundEducation #CLF pic.twitter.com/FjBMvGHdPJ
— Clara Lionel Fdn (@ClaraLionelFdn) February 2, 2018
Mwimbaji huyo aliyezaliwa Barbados ni kama balozi wa kikundi hicho cha kimataifa.
“Kazi yetu haiwezi kuisha,” Rihanna aliwaambia wasikilizaji. “Na hatuwezi kuacha kupigana hadi kila kijana na kila msichana aweze kupata elimu.”
Macron na Rihanna hapo awali walikutana huko jijini Paris nchini Ufaransa ambapo wawili hao walijadili elimu na msingi wake wa kutoa huduma kwa kuendeleza elimu duniani kote.
When I commit, I deliver. @Rihanna, France will always side with those fighting for a better education. #FundEducation pic.twitter.com/9MLGWp2eaS
— Emmanuel Macron (@EmmanuelMacron) February 2, 2018
Mkutano huo umefanyika ili kukusanya fedha kwa ajili ya elimu katika mataifa masikini. Wakati wa mkutano huo, Macron aliahidi kuwa Ufaransa inaweza kuchangia kiasi cha dola milioni 248 na kuwaita viongozi wengine wa ulimwengu kutoa mchango pia.
“Kusaidia elimu sio chaguo ambalo tunaweza kufanya au kutofanya, ni lazima,” Macron alsema hivyo wakati wa mkutano huo”
Na Raheem Rajuu