Habari

Serikali yataja idadi ya vipodozi vilivyosajiliwa kuingizwa nchini

Serikali kupitia Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema kuwa TFDA imesajili jumla ya vipodozi 3179 ambavyo vinavyoruhusiwa kuingiza na kutumika nchini.

Akizungumza leo bungeni mjini Dodoma, Naibu Waziri wa Afya, Dkt. Faustine Ndungulile amesema kuwa katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/217 maeneo 3648 yalikaguliwa ambapo kati ya hayo maeneo 120 yalikutwa na vipodozi ambavyo havina viwango.

“TFDA imekuwa ikichukua hatua zifuatazo kudhibiti uingiaji na utumiaji wa vipodozi. Vipodozi vyote vinatakiwa kusajiliwa kabla ya kibali cha kuingiza nchini kutolewa mpaka sasa TFDA imesajili jumla ya vipodozi 3179 ambavyo ndivyo vinavyoruhusiwa kuingiza na kutumika nchini, TFDA imefungua ofisi 7 za Kanda kwa maana Arusha, Dar es salaam, Dodoma, Mbeya, Mtwara, Mwanza, Tabora kwa lengo la kuimarisha ukaguzi,” amesema Dkt. Ndungulile.

“Katika kipindi cha mwaka wa fedha 2016/017 maeneo 3648 yalikaguliwa ambapo kati ya hayo maeneo 120 yalikutwa na vipodozi ambavyo havina viwango vinavyofaa kwa matumizi ya binadamu na wahusika kuchukuliwa hatua za kisheria.”

Hatua ya ufafanuzi huyo imekuja baada ya Mbunge Mata ally salum Mbunge wa Shauri Moyo aliyeuliza “wananchi wengi hapa nchini hasa wanawake hutumia vipodozi ambavyo havina viwango vinavyofaa kwa matumizi ya binadamu pamoja na jitihada za serikali kuzuia bidhaa hizo Je serikali ina mpango gani madhubuti ya kuzuia vipodozi hivyo.?

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents