Burudani
Siku nikifa wanaonichukia wataomba msamaha kwenye jeneza- Steve Nyerere
Mchekeshaji Steve Nyerere mwenye vipaji vya kuigiza sauti mbalimbali za viongozi ,amefungua akisema kuwa siku akifa wanao mchukia hawataamini na watamuomba msamaha akiwa kwenye jeneza.
Steve kupitia ukurasa wake wa Instagram, alitupia picha za watu mbalimbali wakiwemo mastaa akisema siku akifa watatamani kumuomba msamaha lakini haitakuwa na maana.
Aliweka picha hii kwenye ujumbe huo
“Siku nikifa najua hata wanaonichukia hawataamini, wataniomba msamaha nikiwa kwenye jeneza, lakini itakuwa haina maana, wangine watasema, dah tulimkosea sana na wangine watakuwa wamejifunza kitu kupitia mimi, siku nikifa…,”
Na Emmy Mwaipopo