Burudani

The-Dream aondoka Def Jam Records

Baada ya kukaa kwa miaka saba, mtayarishaji wa muziki na mwandishi wa nyimbo, The-Dream ameondoka Def Jam Records.

ZAEH_DREAM_SHOT04-48gold

Muimbaji huyo aliweka tangazo hilo kwa kuweka logo ya Def Jam na kuandika: I will miss this logo. It all started here! Love Everything that I achieved there, EXODUS THE-DREAM #exodusthedream.”

Akiwa na label hiyo, The Dream alitoa album tano ambazo ni pamoja na LoveHate (2007) Love vs. Money (2009) Love King (2010) Terius Nash: 1977 na IV Play ya mwaka jana.

The-Dream aliteuliwa kuwa Makamu Mkuu wa Rais wa A&R hapo Def Jam mwaka 2012 na ametengeneza nyimbo za wasanii kama Rihanna, Justin Bieber, Mariah Carey na Beyonce. “Let the New Tides bring The Things not yet seen. There’s more where those came from,” alisema.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents