Habari
Tidal ya Jay Z yafikisha watumiaji milioni moja
Jay Z ana haki ya kusherehekea kwa mafanikio yaliyotokana na mtandao wake wa Tidal.
Rapper huyo alitumia Twitter kutangaza kuwa mtandao huo wa kusikiliza nyimbo umefikisha watumiaji milioni moja.
“Nothing real can be threatened, nothing unreal exists. TIDAL is platinum. 1,000,000 people and counting. Let’s celebrate 10/20 Brooklyn,” alitweet.
Tangu ianzishwe, TIDAL imekuwa ikikumbana na vikwazo vingi ikiwa pamoja na viongozi wake wa juu kujiuzulu.