Habari

Video: Watoto hawa hupanda mlima wa mita 800 kila siku kwenda na kurudi shule

Huko China kitongoji cha Sichuan, kwa muda mrefu watoto wamekuwa wakishuka na kupanda mita 800 za mlima kila siku kwenda na kurudi shule kwa kutumia njia za kienyeji ambazo ni ngazi za miti.

Kwa sasa wakazi wa kijiji hicho wameanza mchakato wa kujenga ngazi ya chuma mradi unaotarajiwa kukamilika mwezi November mwaka huu.

Ngazi hiyo ambayo inatarajiwa kuwa na muundo imara zaidi na salama itarahisishia maisha ya wanakijiji hao ambao wamekuwa wanaitumia ngazi hiyo kupanda na kushuka kila wiki kununua bidhaa mbalimbali na kufanya biashara zao katika soko ambalo liko mbali na wanakoishi.

Source: CCTV News

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents