Habari

Vyeti Feki, ngoma bado mbichi – Prof. Ndalichako

Waziri wa Elimu,Sayansi,Teknolojia na Ufundi, Prof. Joyce Ndalichako amesema kwamba suala la uhakiki wa vyeti feki nchini tangu Tanzania ipate uhuru ni mara ya kwanza zoezi la uhakiki kufanyika huku akisema,ngoma bado mbichi.

Profesa Ndalichako, ameyasema hayo mjini Dodoma wakati wa kumkabidhi Rais Magufuli taarifa ya majina ya watumishi wa umma wenye vyeti feki.

“Mheshimiwa Rais, suala la uhakiki wa vyeti umefanyika kwa mara ya kwanza, tangu nchi yetu ilipopata uhuru, tunakupongeza sana kwa kuonyesha uongozi thabiti kwa vitendo. Kwakweli huna kigugumizi katika kufanya maamuzi, na tunakupongeza sana. Mheshimiwa Rais, wizara yangu imetekeleza maelekezo ya serikali kwa kuhakiki vyeti vya kidato cha nne, cha sita na vyeti vya ualimu katika ngazi ya cheti na stashahada kwa watumishi wa umma nchini,”alisema Ndalichako.

“Kwa hiyo naomba mnisikilize vizuri, tumehakiki vyeti vya kidato cha nne na cha sita kwahiyo kwa maneno haya, ngoma bado mbichi maana yake vyeti vya taaluma bado hatuja hakiki. Matokeo tunayoyawakilisha leo (jana) ni ya uhakiki wa vyeti kidato cha nne, cha sita na vyeti vya ualimu kwa watumishi wa umma.”

Aidha Ndalichako aliwaasa wanafunzi wote nchini kusoma kwa bidii, na kuongeza njia zote zimefungwa.

Na Emmy Mwaipopo

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents