Habari
Wanajeshi 11 wa Israel wauawa Gaza usiku
Jeshi la Israel limetoa orodha yake ya wanajeshi ambao wamefariki katika vita vinavyoendelea na Hamas.
Idadi hiyo ya vifo sasa imefikia 326, wakiwemo wanajeshi 11 waliofariki huko Gaza siku ya Jumanne.Wanajeshi hao wote walikuwa na umri wa kati ya miaka 19 na 20.
Picha za jeshi la Israel zinaonyesha majengo yaliyoharibiwa
Jeshi la Ulinzi la Israel limetoa picha za hivi punde za operesheni yao ya kijeshi kaskazini mwa Ukanda wa Gaza.
Picha kadhaa zinaonyesha majengo yaliyoharibiwa na vifusi, ikionyesha ukubwa wa athari za mashambulizi ya anga na mashambulizi ya ardhini ya Israeli.