Michezo
Wanatamani warudi tena – Rais Karia
Rais wa Shirikisho la Mpira wa miguu Tanzania Wallace Karia akiwa kwenye mahojiano leo na waandishi wa Habari anasema “Uzinduzi wa AFRICAN FOOTBALL LEAGUE (AFL) kusema kweli umetubeba wanatamani warudi tena na niseme lile kombe la SUPER CUP ni biashara ile sasa hivi umeona limeenda kuchezewa Saudi Arabia dhidi ya USM Algers na Al Ahly, Kwahiyo wakatamani yani wakaniuliza President zungumza na Makampuni ya kibiashara hapa au serikali yako kwamba tunaweza tukacheza SUPER CUP Tanzania.
Kwa Hali inavyoendelea Uwanja wa Arusha ukiisha tu sisi tutaomba SUPER CUP ichezewe Arusha hii ni sawa na kuileta afrika na Dunia nzima Arusha. Alisema Rais Karia.
Imeandikwa na Mbanga B.