Burudani

‘Wapo’ ni baba lao katika nyimbo zangu zote – Nay wa Mitego

Msanii wa muziki wa hip hop, Nay wa Mitego amedai wimbo wake ‘Wapo’ ni wimbo ambao umefanya vizuri kwa muda mchache kuliko nyimbo zake zote alizowahi kuziachia katika maisha yake ya muziki.

Rapa Nay wa Mitego akiwa kwenye moja kati ya shows zake za hivi karibuni

Akiongea na Bongo5 Alhamisi hii, Nay wa Mitego amesema hata show zake zinajaza zaidi kuliko kipindi cha nyuma kutokana na wimbo huo.

“Nimeshatoa nyimbo zikawa kubwa, nimeshatoa nyimbo watu wakawa wanaimba, nimeshotoa nyimbo zikawa gumzo lakini ‘Wapo’ ni kiboko,” alisema Nay wa Mitego.

Aliongeza, “Ni wimbo ambao umefanya vizuri kila sehemu hata kwenye show mikoa yote niliyozunguka mambo yamekuwa ni mazuri sana. Kwahiyo naweza kuthubutu kusema Wapo ni kazi kubwa kuliko hata kazi zangu zote,”

Rapa huyo ambaye anatarajia kufanya show ya ‘Wapo Night’ mwezi huu katika ukumbi Dar Live jijini Dar es salaam, amewataka mashabiki wake kukaa mkao wa kula kwaajili ya remix ya wimbo huo.

Katika hatua nyingine, rapa huyo amewataka mashabiki wa muziki wake kuendelea kumsupport msanii wake mpya B-Gway ambaye anafanya vizuri na wimbo wake mpya uitwao ‘Sijachukua’.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents