Watu saba wafariki baada ya ndege ya jeshi kupata ajali karibu na uwanja wa ndege wa Abuja (+ Video)
Watu saba wamefariki baada ya ndege ya jeshi la Nigeria kuanguka muda mfupi baada ya kupaa kutoka uwanja wa ndege, katika mji mkuu wa Abuja, asubuhi ya Jumapili, kwa mujibu wa maafisa.
Ndege hiyo ya jeshi la anga la Nigeria iliripoti kukumbwa na hitilafu katika injini yake, msemaji wa Air Vice Marshal Ibikunle Daramola, aliandika katika Twitter yake.
Aliongeza kuwa ndege hiyo ilikuwa njiani kuelekea Minna, kaskazini mwa jimbo la Niger.
Mkuu wa wafanyakazi wa shirika la ndege hiyo ameagiza uchunguzi kufanywa mara moja.
Katika msururu wa ujumbe wa Twitter, vikosi vya angani vimetoa wito kwa watu “kuwa watulivu na kusubiri matokeo ya uchunguzi”.
AIRCRAFT ACCIDENT
This is to confirm that a Nigerian Air Force (NAF) Beechcraft KingAir B350i aircraft crashed while returning to the Abuja Airport after reporting engine failure enroute Minna. First responders are at the scene. Sadly, all 7 personnel on board died in the crash
— Air Vice Marshal Ibikunle Daramola (@KunleDaramola3) February 21, 2021
Mwisho wa Twitter ujumbe, 1
The Chief of the Air Staff (CAS), @CAS_IOAmao, has ordered an immediate investigation into the incident. While urging the general public to remain calm & await the outcome of investigation, the CAS, on behalf of all NAF personnel, commiserates with the families of the deceased.
— Air Vice Marshal Ibikunle Daramola (@KunleDaramola3) February 21, 2021
Mwisho wa Twitter ujumbe, 2
Msemaji wa jeshi la anga la Nigeria amesema abiria wote wamefariki.
Walioshuhudia ajali hiyo waliripoti kuona ndege ikizunguka katika eneo ilipotokea ajali kabla ya kuanguka na kushika moto karibu na barabara ya ndege ya uwanja huo. Wanasema walisikia mlio mkubwa kabla ya ndege hiyo kulipuka na kushika moto.
Mashuhuda mwingine ameiambia shirika la habari la Reuters kwamba harufu ya ndege iliyochomeka na kemikali ilisheheni sehemu ilipotokea ajali hiyo, nje kidogo ya au la uwanja wa ndege.
Bofya hapa kutazama.