Habari

Waziri aliyehusishwa na ubakaji atumbuliwa Ufaransa

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron amemwachisha kazi waziri aliyetajwa katika uchunguzi wa ubakaji, katika mabadiliko ya baraza la mawaziri baada ya muungano wake tawala kupoteza wingi wa viti katika uchaguzi wa bunge.

Ikiwa tu ni mwezi mmoja na nusu baada ya mabadiliko yaliyopita, mawaziri wa mambo ya kigeni, fedha na ulinzi walibaki katika nyadhifa zao lakini Macron alifanya mabadiliko katika nyadhifa nyingine muhimu.

Mkurugenzi wa shirika la Msalaba Mwekundu la Ufaransa Jean-Christophe Combe ameteuliwa kuwa waziri mpya wa mshikamano na uwiano wa kijamii baada ya tuhuma dhidi ya Damien Abad, ambaye anakanusha kufanya kosa lolote, katika kashfa ambayo imeiaibisha serikali.

Mchumi mkuu wa Shirika la Ushirikiano wa Kiuchumi na Maendeleo Laurence Boone ameteuliwa kuwa waziri mpya wa masuala ya Ulaya.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents