Habari

Waziri Kigwangalla aahirisha ‘press conference’ ya kutangaza wanaojihusisha na ushoga

Naibu waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Khamis Kigwangalla, amesema kuwa hawatokuwa na press conference ya kutangaza majina ya mashoga wanaojiuza na kujitangaza mitandaoni.

Waziri huyo aliahidi kutangaza majina na mashoga ambao wanatuhumiwa kujiuza mtandaoni kinyume na sheria.

Jumatatu hii waziri huyo alitoa taarifa ya kuahirisha kutaja majina hayo kwa madai kuna matatizo ya kiufundi.

“Tunaomba radhi hatutokuwa na press conference kuhusu kutangaza majina ya mashoga wanaojiuza mitandaoni kwa sababu za kiufundi!,” alitweet Kingwangala.

Hata hivyo hakuweka wazi kama itafanyika tena.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents