Burudani

Imani ni wimbo wa kuwapoza walioumizwa kimapenzi – Linah

Linah amesema wimbo wake mpya, Imani ni kwaajili ya kuwapoza wale walioumizwa kimapenzi.

13413476_2061420370750172_655622282_n

Akiongea na Bongo5 Linah amesema, ” Unajua kila siku tunaimba furaha sana katika mapenzi, je tunawaangalia vipi wale ambao hawana furaha katika mapenzi? Nikaona niimbe wimbo ambao utawatia moyo katika mahusiano yao ambao huwa wanatengwa na familia. Unakuta wanaambiwa kuwa huyo mwanaume maskini, sijui mbaya, unakuta mwingine labda anaambiwa naye mwanamke wako mbaya. Kwa wimbo huu watu kama hao wakiusikiliza wanafarijika sana.”

Kuhusu kurudi kwenye muziki wa injili, Linah amesema, “Kwakweli sina uhakika kwa sasa kama Mungu atanibariki nitaweza au la maana ndio nilipoanzia huko kwahiyo sijajua huko mbeleni.”

Related Articles

Check Also
Close
Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents