Siku ya jana Bongo5 tuliripoti juu ya staa wa muziki kutoka nchini Nigeria @wizkidayo kuuza tiketi zote katika ukumbi mkubwa zaidi nchini Ufaransa ukiopo katika jiji la Paris.
Sasa usiku wake Show ilifanyika na balaa likawa kubwa sanaa.
Hivi ndivyo @wizkidayo alivyotua kwenye show yake hiyo katika ukumbi huo wa Accor wenye uwezo wa kuingiza watu 20,300.
Mpe neno moja Wizkid 🤓🤔
Show ya jana usiku ya @wizkidayo katika ukumbi wa Accor jijini Paris Ufaransa 🔥🔥🔥 pic.twitter.com/iA2sDrGCKh
— bongo5.com (@bongofive) September 17, 2022
Show ya jana ya Wizkid inaingia kwenye rekodi ya kuwa moja ya show kubwa sana ambazo @wizkidayo amewahi kuzifanya duniania.
@wizkidayo ameingia kwenye orodha ya wasanii 8 kutoka Afrika ambao wamewahi kuujaza ukumbi wa Accor Arena.
Wasanii hao ni:
1. Koffi Olomide.
2. Papa Wemba
3. Werrason
4. JP Mpiana
5. Youssou Ndour
6. Fally Ipupa
7. Burna boy
8. Wizkid.