Burudani
Wizkid kuwasaini Efya, R2Bees na Mr Eazi kutoka Ghana kwenye label yake ya ‘Starboy Worldwide’
Msanii wa Nigeria, Wizkid ametangaza kuwasaini wasanii wa Ghana Efya, R2Bees na Mr Eazi kwenye label yake ya ‘Starboy Worldwide’
Wizkid aliwatangaza wasanii hao wanaofanya vizuri huko kupitia Twitter muda mfupi baada ya kutumbuiza kwenye Ghana Music Awards ambapo pia alibeba tuzo ya msanii bora wa Afrika.
Wizkid ambaye ameshika nafasi ya 12 katika chart ya wasanii ambao nyimbo zao zinapakuliwa zaidi kwenye mitandao ya iTunes na Spotify, alimtangaza pia rais mpya wa label yake.
Hii ni chart ya wasanii wanaoongoza kwenye mtandao wa iTunes na Spotify