Burudani
50 Cent apewa leseni ya upromota wa masumbwi
Rapper wa G-Unit, 50 Cent ameongeza ‘title’ mpya kwenye CV yake kutokana na ripoti zinazosema kuwa weekend hii jamaa amekabidhiwa rasmi leseni ya upromota wa ndondi katika jimbo la New York.
Kwa mujibu wa ripoti, Fif anatafuta pia kibali kingine kwenye jimbo la Nevada.
Mwandishi wa jarida la Sports Illustrated, Chris Mannix anaripoti kuwa kampuni yake inaitwa The Money Team Promotions (TMT) na anashirikiana na rafiki yake kipenzi Floyd Mayweather.