Habari
Abdul Nondo ile kesi yake ya kujiteka, aachiwa huru na Mahakama ya Mkoa wa Iringa
Mahakama ya Mkoa wa Iringa leo Novemba 05, 2018 imemuachia huru aliyekuwa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo.
Mnamo mwezi Agosti 27 mwaka huu, Mahakama hiyo ilimkuta Nondo na kesi ya kujibu kwa mashtaka ya kusambaza taarifa za uongo akidai kutekwa, huku ikimtaka alete mashahidi watano kwenye utetezi wake.
Abdul Nondo alikuwa anakibiliwa na kesi ya kutoa taarifa za uongo kuwa alitekwa na watu wasiojulikana mapema mwanzoni mwa mwaka huu.
Nondo ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), kabla hajasimamishwa masomo kutokana na kesi hiyo, alidaiwa pia kutoa taarifa za uongo kwa polisi katika Kituo cha Mafinga mkoani Iringa.