Habari
AFCON 2013: DRC watoshana nguvu na Ghana, Mali waitandika Niger
Goli la mwisho mwisho la nahodha wa Mali Seydou Keita liliupa jana ushindi timu yake dhidi ya Niger kwenye kombe la mataifa ya Afrika linaloendelea nchini Afrika Kusini.
Mchezaji huyo wa zamani wa Barcelona aliweka wavuni goli hilo zikiwa zimebaki dakika 6 tu baada ya mchezo huo kuonesha dalili ya draw nyingine ya nne.
Ushindi huo umeiweka juu Mali kwenye kundi B, baada ya Ghana na DR Congo kutoka sare ya 2-2.Leo timu za kundi C zinaingia uwanjani ambapo Zambia itakutana na Ethiopia na Nigeria ikicheza na Burkina Faso.