Burudani
Aliyebeba mimba ya Kanye West afikisha miezi tatu
Ikiwa imepita miezi kadhaa tangu rapper Kanye West na Kim Kardashian kutangaza kumlipa mtu kwa ajili ya kubeba mimba hatimaye jambo hilo limefanikiwa baada ya mwanamke aliyelipwa kufikisha miezi mitatu ya ujauzito.
Kim ambaye anadaiwa kutokuwa na uwezo wa kubeba mimba nyingine, walimlipa mwanamke huyo zaidi ya dola 4500 kwa ajili ya kubebea mimba itakayowaletea mtoto wa tatu.
Mtandao wa Us Weekly umebaini kuwa wakati Familia ya West inatoa taarifa juu aya kumpata mbeba mimba mwezi Juni tayari walikuwa wameshajua mpata na kumpandikizia mbegu mtu huyo.
Mwanamke huyo amekuwa akifanya kazi hiyo kwa watu mbalimbali na anatarajiwa kujifungua mtoto wa tatu wa Kim na Kanye ifikapo Januari mwakani.
Na Laila Sued