Habari
Audio: Tamko la serikali kuhusiana na mlipuko wa bomu Arusha lilitolewa na Waziri wa nchi
Serikali kupitia Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, William Lukuvi leo bungeni imetoa tamko lake kuhusiana na tukio la juzi, June 15 jijini Arusha la mlipuko wa bomu kwenye mkutano wa CHADEMA uliosababisha vifo vya watu wawili na kujeruhi wengine zaidi ya 60.
Waziri William Lukuvi
Katika tamko hilo, serikali imeunda tume ya kuchunguza mlipuko huo wa bomu itakayoongozwa na Mkuu wa Operesheni na Mafunzo, wa Jeshi la Polisi Kamanda Paul Chagonja na pia kutenga shilingi milioni 100 kama zawadi kwa wananchi watakaotoa taarifa za siri kuhusiana na wahusika wa tukio hilo la kigaidi.
Msikilize zaidi hapa.