Burudani

BBA Updates: Upweke wamuandama Feza Kessy, atasurvive bila Oneal?

Inaoenekana upweke mkali unamuandama Feza Kessy baada ya mpenzi wake Oneal kutoka jana kwenye shindano la Big Brother Africa, The Chase.

Feza

Asubuhi ya leo Feza ameonekana akiwa na upweke wa kufa mtu na kuuchapa usingizi wa pono huku kitanda kilichozoea watu wawili kikionekana kupwaya. Kuondoka kwa Oneal kunamwacha Feza peke yake hasa kwakuwa mara nyingi alikuwa akitumia kuwa pembeni ya ubavu wa Mtwasna huyo.

Jana baada ya Oneal kupigwa kibuti na BBA, Feza alielekea juu na kukaa mwenyewe huku akibubujikwa na machozi baada ya kuanza kuukosa uwepo wa Oneal.

Kwakuwa Oneza imekufa rasmi jana, nani atakuwa karibu tena na Feza? Ataweza kuendelea na mchezo huo wa kufukuzana aka The Chase mwenyewe? Ama siku zake ndio zinahesibika?

Kwa upande mwingine, jana Uganda iliamua kutompigia kura Feza na kumpa kura yake Bimp. Waganda wanasema wamefanya hivyo makusudi kulipiza kisasi.

“When LK4 and Denzel were evicted where was team EAC? Denzel had to get votes from south africa instead. Uganda does not owe anyone and anyways this isnt a game of regionalism for Pete’s sake,” anasema Vuyolwethu Vema Ndlovu.

“Plus Denzel was the best rep from EA this year and they didn’t support him and they want Uganda to be loyal,” anasema Danny Lanzy.

Ogwado La Quintus Joachim wa Makerere University anasema: U Tanzanians put LK4 N DENZEL up for eviction.. What r u talking about.. N it was only SA tht stood with us evn with LK4 and KYLE.. We hv always been loyal to u.. While u continuously stab us in the back.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents