Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) imetoa gawio kwa serikali la Sh. Bilioni 18.9 ikiwa ni utekelezaji wa jambo hilo kwa mujibu wa kifungu cha 10 cha sheria ya Msajili wa Hazina sura 370.
Gawio hilo la Brela limetolewa leo Ikulu jijini Dar es Salaam na kupokelewa na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan wakati wa halfa ya kupokea gawio kwa amshirika ya umma na binafsi ambayo imehudhuria na viongozi mbalimbali akiwemo Mjumbe wa Bodi ua Ushauri ya Wizara kwa Brela Dk. Fred Msemwa na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Brela Godfrey Nyaisa.