Habari
Bulaya aibuka mshindi kesi ya uchaguzi
Mahakama kuu kanda ya Mwanza imetupilia mbali kesi ya uchaguzi ya kupinga ubunge wa Bunda mjini na kumpa ushindi Ester Bulaya wa Chadema.
Baada ya Mahakama kutupilia mbali kesi hiyo Mbunge huyo wa Bunda Mjini kupitia facebook ameandika:
“Nimemshinda Wasira kwa wananchi na leo nimemshinda mahakamani mahakama imetupilia mbali kesi yake dhidi ya. Ushindi wangu”
Kesi hiyo ya kupinga matokeo ya uchaguzi ilifunguliwa katika Mahakama Kuu kanda ya Mwanza lakini ilikuwa inasikilizwa Mjini Musoma.
BY: EMMY MWAIPOPO