Habari
Dar ni foleni kali ya magari, mgomo wa madereva wa daladala na mvua (Picha)
Wakazi wa Dar es Salaam leo wamekiona cha mtema kuni baada ya kero zaidi ya tatu kuunganika na kuleta usumbufu mkubwa.
Mgomo wa madereva wa magari abiria, umewafanya wananchi wengi ama kutumia gharama zaidi ya kufikia maeneo waliyokuwa wakienda kwa kutumia bodaboda na bajaj au kutembea kwa maguu.
Kumeshuhudiwa misululu mikubwa barabarani ya wakazi wa Dar wakitembea kwa mguu kutokana na mgomo huo. Kama haitoshi mvua iliyoanza kunyesha tangu asubuhi nayo imesababisha misululu mirefu ya magari katika maeneo mengi ya jiji.
Foleni hiyo imekuwa kali zaidi kuanzia jioni. Hizi ni baadhi ya picha za foleni hiyo.