Michezo
David Moyes kuwa kocha wa Real Sociedad ya Hispania?
Klabu ya Hispania, Real Sociedad imemfukuza kocha wao Jagoba Arrasate siku ya Jumapili baada ya kufungwa na Malaga siku ya Jumamosi. Chaguo lao la kwanza kuziba nafasi hiyo ni kocha wa zamani wa Manchester United na Everton, David Moyes.
Moyes kwa sasa yupo nchini Qatar, ambapo anafanya kazi BeIN Sports, na inaeleweka kuwa anafikiria nafasi hiyo.
David Moyes 51, anafahamu kuwa ana tahadhari kubwa kwani anajua kazi ijayo inahitaji mtu sahihi baada ya kipindi kigumu cha miezi 10, Old Trafford.