Habari
D’Banj ashoot video ya wimbo wake mpya, ‘Bachelor’ jijini Atlanta
Koko Master yupo kwenye matawi marefu zaidi sasa hivi kwakuwa tayari anamiliki mjengo wake mwenyewe jijini Atlanta, Georgia nchini Marekani.
Hivi karibuni ameamua kushoot video ya wimbo wake mpya uitwao Bachelor katika jiji hilo huku director akiwa Sesan Ogunro.
Katika wimbo huo D’Banj anaelezea kwanini anapenda kuishi maisha ya ukapela.
Story ya video hiyo inaanza kwa kuonesha mpenzi wake anayeenda kwa hasira kwenye nyumba yake bila sababu yoyote lakini badala ya D’Banj kukosa raha anaamua kuita gari kubwa lililojaa mademu wakali na kuja kula bata naye.