DC Jerry Muro aanza kazi kwa kasi, akamata Malori 10 kutoka Kenya ‘hii ndio kazi niliyotumwa’ (+video)
Mkuu wa Wilaya ya Arumeru Mhe. Jerry Muro amefanya zoezi la ukaguzi wa malori 10 yaliyokuwa yakitokea Nchi jirani ya Kenya.
Mara baada ya kuyatilia mashaka Malori hayo kutoka Mombasa kupitia njia ya Namanga tukio ambalo limeonekana sio la kawaida Kwa magari hayo kupitia njia ndefu ya Namanga kutoka Mombasa kwenda Dar es salaam.
DC Muro akiwa katika majukumu yake Siku ya Jumapili Jioni alishangazwa na kitendo cha Malori hayo mapya kupita katika Wilaya yake kwa kutumia boda ya Namanga badala ya kupitia Tanga mida ya jioni yakiwa na *chesses number* ambazo alizitilia mashaka.
Muro amesema amewaagiza Maofisa TRA kuyagua Malori hayo ili kujiridhisha kutokana na kuwepo Kwa tetesi za baadhi ya wafanyabiashara wasio waaminifu kutaka kuhujumu Bandari za Tanzania na kukimbilia Nchi Jirani kutokana na Bandari za Tanzania kuwa na udhibiti mzuri wa Vitendo vya Magendo na Rushwa .
DC Muro ameahidi kuwa katika Wilaya anayoiongoza ya Arumeru Kamwe haitakuwa uchochoro wa kupitisha bidhaa haramu za magendo kutoka Nchi Jirani.
Ajiangalie asifanye Kz kwa sifa ili kumfurahisha magu bila kufuata sheria itakula kwake magu hana ushoga na mtu
💊💊💊💊💊💊💊💊💊
alitumwa akamate maroli hehehe hv tupo epsodi ya ngapi
Afadhari Nikajua umetumwa kumnyong’onyesha upinzani… ubarikiwe
tokea igunga mjini tupo pamoja sana mpakatamati yakipindi hiki
Niliwahi kusoma makala fulani siku moja ikielezea kuwa ushamba ni mbaya sana kushinda ULIMBUKENI!