Habari
DC Jokate na Mimba za Utotoni: Kuna mzee wa miaka 85 amemlawiti kijana wake (Video)
Mkuu wa Wilaya ya Kisaware Mhe Jokate Mwegelo amewataka wakazi wa Kisarawe kuwalea vyema watoto wao wa kike na kuwaepusha na mimba za utotoni huku akionesha kuchukizwa na tukio la mzee wa miaka 85 kumlawiti kijana wake ambalo limetokea Wilayani humo.
Ameyasema hayo Alhamisi wakati akizindua mradi wa shule ya msingi Kora, kata ya Kazimzumbwi ambapo wamewataka wazazi wa watoto wa maeneo hayo kuhakikisha watoto wao wanakwenda shule.