Burudani
Diddy akamatwa na polisi kwa kumdunda kocha wa mpira
Diddy amekamatwa na polisi kwa kudaiwa kupigana na kocha football wa chuo kikuu cha California, UCLA.
Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ, polisi wa chuo hicho walimkata rapper huyo tajiri jana.
Mtoto wa Diddy, Justin Combs anachezea kwenye timu ya UCLA. Kocha msaidizi alikuwa akimkalipia Justin uwanjani na Diddy hakupenda kiasi cha kumfuata na kutaka kumdunda.
Anaendelea kushikiliwa kwenye kituo cha polisi cha chuo hicho.