Burudani

Dully Sykes: Sishangai ugomvi wa Alikiba na Diamond, nashangaa wa TID na Q Chillah

Dully Sykes amedai kushangazwa kusikia watu wazima kama TID na Q Chillah wakilumbana kwa jambo la miaka mingi iliyopita na kwamba mambo kama hayo wanapaswa kuwaachia wadogo zao mathalan Alikiba na Diamond.

Dully Sykes na TID

Dully ameiambia Bongo5 kuwa TID na Q wamemfedhehesha.

“Hawa ni watu wazima,” amesema Dully. “Mimi kama kuwazungumzia ninawazungumzia Diamond na Alikiba. Hawa ni vijana, kwanini Q Chillah na TID wasimalize masuala yao? Wanashindwa kuweka pembeni tofauti zao! Kwanini wanagombana wakati ni watu wazima tayari?

“Sishangai ugomvi wa Alikiba na Diamond nashangaa ugomvi wa TID na Q Chillah kwasababu Diamond na Alikiba ni watoto! Mimi nitashangaa TID kugombana na Q Chillah kwasababu wao ni watu wazima. Wanatakiwa wapatane ili watoto kama Diamond na Alikiba wapatane. Mimi siwezi kuzungumza nao chochote waache wagombane.”

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents