FIFA watangaza majina matatu ya wachezaji watakaowania tuzo ya mchezaji bora wa dunia, Lionel Messi atoswa
Shirikisho la Soka Ulimwenguni (FIFA) limetangaza majina matatu ya wachezaji watakaowania tuzo ya mchezaji bora wa dunia kwa mwaka 2017/18, ambapo kwenye majina hayo mshambuliaji wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi ametoswa kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2006.
Majina ya wachezaji hao ni Luka Modric (Real Madrid), MO Salah (Liverpool) na Cristiano Ronaldo (Juventus). Majina hayo ndiyo yale yale yaliyotangazwa kwenye tuzo ya mchezaji bora wa kiume barani Ulaya.
Maswali mengi yameibuka mitandaoni kwanini Lionel Messi ameachwa kwenye orodha hiyo, ile hali yeye ndiye mfungaji bora barani Ulaya msimu uliopita na ameisaidia timu yake ya Barcelona kuchukua ndoo ya La Liga na kombe la Mfalme ‘Copa Del Rey’.
Bado haijajulikana wameangalia nini kwani mchezaji kama MO Salah timu yake ya Liverpool haijachukua kombe lolote huku yeye akiibuka mfungaji bora wa EPL.
Duh mwisho wa zama zao umefika
Kutesa kwa zamu mess labda South America
Watajuta fifa
Khaaaa yan kawekwa ronaldo badala ya hazard duuuh kwel noma kwakwel
Sasa hazard wamueke kwa vigezo gani kuwa mshindi wa 3 world cup au kutolewa na Barcelona
Huy salah na ronaldo wamewekw kwa vigez vp hem ntajie na mpra alchz hadrd unafanana na wa ronaldo na salah kweny world Cup
Ajipange upy
Duuh Hazard tena? Bora hata ungesema MBAPE
ivi unazani kuwa top score #uefa #ucl ni kitu kidogo? jua kuwa kule akunaga cha #stoke_city wala #west_brow
dauda tym nyngne uwa unazngua kidogo mesi ana kigezo cha kuingia top 3 kama mfngaj bora hispain tyu na mfungaji bora uefa ni ronaldo alaf uefa walifka wp
Next time kina MBAPE watahusika..hawa muda wao tayari umeisha
Dauda huku umemtoa wap wew?