Burudani
Hamza Kalala awasihi wasanii wa Bongo Flava kufanya muziki wa live
Mwanamuziki mkongwe nchini, Hamza Kalala amewasihi wasanii wa muziki wa Bongo Flava kuacha kutumbuiza kwa CD na badala yake kufanya muziki wa live.
Hamza Kalala ambaye amewahi kufanya kazi na wasanii wa muziki wa kizazi kipya akiwemo Lady Jaydee ametoa ushauri huo kupitia E-News ya EATV.
“Nimeshawahi kufanya kazi na wasanii wa THT na Lady Jaydee, hawa wanapiga dansi vizuri kabisa hawana matatizo kabisa, sema kuna sijui hii kizazi kipya, sema napiga muziki kutokana na wakati uliopo lakini sio kizazi kipya,” alisema.
“Mimi nawashauri tu vijana wapige hiyo hiyo style yao ya Bongo Fleva lakini wapige tu muziki wa live na sio CD.”