Habari

Hapa Kazi Tu: RC Ayoub wa Mjini Magharibi azidi kuwa kivutio Zanzibar

Jumamosi hii kampeni ya Mimi na Wewe imezidi kupamba moto kutoka kisiwani Zanzibar ikiongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi Ayoub Mohamed Mahmoud.


RC Ayoub Mohamed Mahamudu akishiriki katika ujenzi.

Akiwa katika Wilaya ya Magharibi A, Mkuu
wa Mkoa huyo ameendelea kushirikiana na wananchi wa sehemu hiyo kuendeleza madarasa ya Shule ya Msingi Sharifu Msa, ambapo yaliachwa kwa muda wa miaka kumi bila kuendelezwa.

Kampeni ya Mimi na Wewe ilizinduliwa Mwezi Mei 21 Mwaka huu na Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu.

Na Laila Sued na Salum Kaorata

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents