Habari

Hapa pesa kwanza, halipendwi shirika inapendwa pesa – Rais Magufuli

Rais John Pombe Magufuli amemtaka Msajili wa Hazina , Ndg. Athumani Mbuttuka kuhakikisha anatumia sheria aliyopewa na serikali pamoja na Bunge dhidi ya mashirika ambayo hayashiriki kwenye kujenga uchumi wa nchi haswa katika ulipaji kodi na utoaji wa gawio kwa serikali.

Rais Dkt. John Pombe Magufuli

Rais Magufuli ametoa kuli hiyo mapema leo wakati akipokea gawio kutoka kwa Wakala, Kampuni Taasisi na Mashirika ya umma, kwa mwaka wa fedha 2017/2018, ambapo amemtaka Msajili kutazama kama atawafukuza viongozi wa mashirika, kuyafuta au kuwafilisi kulingana na sheria inavyomuongoza.

Rais Magufuli amesema katika uwekezaji uliofanywa na serikali wa zaidi ya shilingi trilioni 49, kisha kuja kupokea kiasi cha gawio kiasi cha bilioni 736 ni dogo sana kitu ambacho si sahihi.

Magufuli amesema uongozi wa mashirika hayo ubadilishwe au shirika lifutwe kwa kuwa hakuna haja ya kuwepo na mashirika jina ambapo ameongeza kwamba “ni nafuu usiwe nacho kuliko kuwa na kitu kichoshiriki kwenye kujenga uchumi”.

“Hakuna haja ya kukaa na mashirika ambayo yapo tu kwa jina. HAPA PESA KWANZA. Halipendwi shirika inapendwa pesa” amesema Rais Magufuli.

Wakati huo huo Rais ameyapongeza mashirika 47 yaliyoweza kutoa gawio jumla ya Bilioni 7 ambapo amewataka mashirika ambayo hayajatoa hata shilingi waanze kuona aibu.

Related Articles

7 Comments

  1. I am a great spiritual helper. My brother try to make good use of this opportunity that has been given to you because opportunity comes but ones. I am here to help you with the following ; 1. Instant money 2. Pocket no dry 3. Pot money 4. Money rituals 5. Promotion in office 6. Promotion at work place 7. Promotion at every business 8. Lotto numbers 9. Lotto lucky 10. Scam lucky 11. Boy /Girl lucky 12. Husband /Wife lucky 13. Herbal treatment 14. Low sperm count 15. Sex power 16. Success every and so on if any problem you can call me on this number 0550570377 or add me on Whatsapp +223550570377 and your problems are solve

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents