Burudani
Hasara aliyoipata Roma baada ya uvamizi Tongwe Records
Msanii Roma Mkatoliki amesema uvamizi wa studio za Tongwe Records umempelekea kupoteza nyimbo nyingi ambazo ni zaidi ya albam moja.
Roma amesema kutokana na hasara hiyo, kwa sasa bado hayupo tayari kutoa wimbo mpya kutokana na muziki kuwa ni hisia na kwa sasa hayupo katika mazingira hayo.
“Albam kabisa, ni kama material ya kutoka mwaka 2012/13 kushuka huku chini mengi yamesepa ndio maalbam ya kipindi kile. Na always tunasema muziki ni hisia, kwa hiyo hatuko kwenye mazingira comfortable ya kuchukua kalamu na karatasi na kuanza kuandika vitu, nikirelax naweza nikatoa (wimbo), kwa hiyo sasa hivi muendelee kurequest na kupiga Usimsahau Mchizi,” Roma alikiambia kipindi cha XXL.
By Peter Akaro