Habari

Huyu ndio Rapper aliyepoteza maisha jana kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya

Huyu ndio Rapper aliyepoteza maisha jana kutokana na matumizi ya madawa ya kulevya

Malcolm James McCormick a.k.a Mac Miller alizaliwa miaka 26 iliyopita January 19, ya mwaka 1992 katika mitaa ya Pittsburgh, Pennsylvania nchini Marekani.Licha ya kuwa rapper na mwimbaji mac aliwahi kuwa producer chini ya pseudonym.

Mapema mwanzoni mwa mwaka 2010, Miller alisaini mkataba na studio ya rekodi ya indie ya Pittsburgh ya Rostrum Records. Hatimaye alianza kurekodi albamu yake ya kwanza ya studio Blue Slide Park, na kuiachilia mnamo Novemba 8, 2011. Albamu hiyo ilifanikiwa kuwa nambari moja kwenye chati ya Billboard 200 ya Marekani, na kuifanya kuwa wa kwanza kufanikiwa kuingiza albamu na kuwa ya kwanza kwenye chati tangu Album ya Tha Dogg Pound ya 1995,iliyojulikana kama Dogg food.

Mwanzoni mwa mwaka 2013, Miller alizindua rekodi lebo yake iliyojulikana kama Remember Music, iliyoitwa jina la rafiki yake ambaye alikufa. Albamu ya pili ya Miller, ya Watching Movies na Sound Off, ilitolewa tarehe 18 Juni 2013. Mnamo Januari 2014, Miller alitangaza kuwa hafanikiwa kusaini tena kwa Rostrum Records.na Oktoba 2014, iliripotiwa Miller amesaini mkataba na rekodi lebo yake na studio yake remember music, pamoja na Warner Bros. Records.

Septemba 7, 2018 Miller alitaarifiwa kuwa amekufa kwa kujioverdose na madawa ya kulevya katika nyumba yake ambaye alikuwa kwenye Studio. jamaa ameiaga dunia akiwa na umri wa miaka 26. taarifa za awali zilisema kuwa  mgonjwa amekufa kwa kukamatwa na mshtko wa moyo, kulingana na wito uliotolewa baada ya kupigiwa namba ya msaada  911. na baada ya mamlaka husika kuwasili Miller alitangazwa kuwa amekufa kwenye eneo hilo.

Hiyo ndio historia ya Mac Miller kwa ufupi.

By Ally Juma.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents