Ifike mahali turuhusu mtu akihama chama ahame na ubunge wake – Nape Nnauye
Mbunge wa jimbo la Mtama tiketi ya CCM, Nape Nnauye amefunguka kuzungumzia hama hama ya wabunge na madiwani wengi kutoka nyama vya upinzani kwenda chama tawala cha CCM.
Malalamiko ya wengi katika mitandao ya kijamii yanadai kwamba hama hama hiyo imeweza kuisababishia serikali gharama kubwa za kurudia uchaguzi.
Akiongea na Azam TV Ijumaa hii, Mhe Nape amedai ingawa ni jambo gumu lakini angependa wabunge ambao wanahama vyama waruhusiwe kuendelea na nafasi zao kwa kuwa wamechaguliwa na wananchi.
“Hii kitu nadhani ina ukakasi, najua haivunji sheria lakini ina ukakasi na kama ina ukakasi nadhani umefika wakati pengine tukatengeneza forum ya kupitia sheria zinazoongoza huu mchezo kwenye mfumo wa vyama vingi,”
“Kwa mfano ifike mahali turuhusu mtu akihama, ahame na ubunge wake”
Wiki iliyopita tulishuhudia mbunge wa Ukonga Mwita Waitara akihama CUF na kuhamia CCM na wiki hii kamati kuu ya chama hicho imempitisha kugombea ubunge.
Ifike mahali kusiwe na wabunge
kweli kabsa
Nikweli pesa nyingi inapotea alafu wanajiita wazalendo
Bora hivyo kuliko uchaguz kila siku
Porojo,
Tujenge hoja ya mgombea binafsi
Kabisaa maana wananchi tunapata hasara sanaaa … Watu wanaumia wanakufa Na mengine chungu nzimaa
jambo jema sana
Chama chako hakiwezi kukubali sababu hiyo hoja haitofautiani na mgombea binafsi. Huko kwenu mkismbiana ukweli hutishiana kufukuzana
Hiyo mbaya, mgombea akihama chama au akifa mshindi wapili katika kinyang’nyilo mdio achukue nafasi hii itapunguza wimbi lakutia hasara wananchi.
Stupid
100% IQ yako ipo juu sana.
Ni kweli kuhama chama au kufukuzwa uanachama isiwe sababu ya mtu kupoteza ubunge wake.
mtu akijiuzulu ubunge. udiwani. atoe yeye ela zake kuludia uchaguzi kama utaona atakae jiuzulu thubutuuu
Chama tawala cha huyo mbunge aliyehama chama kiteuwe mbunge mwengine
Unajua kipindi unapigiwa kura,kuna wapiga kura wa aina kama tatu hivi mosi..kuna wapiga kura wa mapenzi ya yachama,yaan anakupigia kura kwa sababu anakipenda chama pil kuna mpiga. Kura kwa mapenzi ya mtu husika (mgombea)na 3..kuna wapiga kura wa mizuka yaan yeye anafuata mkumbo…sasa je wale wa mapenzi ya chama utakuwa umewatendea haki
Sehemu ya maisha tu.
Hiyo safi hapo umenena .
Kweli
Huyu jamaa ni kama zile sinema za kudaka Risasi…😆😆😆
Hayo ndio maneno
Kamaanisha wanatia hasara kodi za wananchi bora kama vipi wakihama chama weather wagharamie uchaguzi kwa Pesa zao za mifukoni au ikishindikana basi waruhusiwe kuhama na ubunge wao ili kuepuka kuwaumiza wananchi wabaolipa kodi zao kwa maendeleo ya kijamii na nchi kwa ujumla na sivyo unavyofikiria wewe
Kwa kweli wanasiasa !!!.
Akihama chama apoteze ubunge na kama atataka tena ubunge basi ghalama za uchaguz zimhusu…🤔🤔🤔
Sio ahame na ubunge wake akihama asubiri mwaka wa uchaguz ndo agombee tena
Haswa👍
Hapana….hapana,binafsi hilo halitasaidia,napendekeza iwe hivi,kama mtu akihama chama basi yule aliyemfuata yaan wa pili wakati wa uchaguzi ndo awe mbunge bila kujari chama.
La sivyo watu watahama mala 20.
Mtu akitaka kuhama wakati ni mbunge ashitakiwe kwa kuisababishia serikali hasara,haiwezekani mtu ahame chama apoteze ubunge,then achukue fomu aombe ubunge tena.Ni dharau sana.
Umemaanisha katiba mpya
Sikia hili zuzu lingine huku
Bora aise