Jaguar aibua jipya lingine nchini Kenya, Vijana wampongeza wazee roho juu
Mbunge wa Jimbo la Starehe nchini Kenya, Jaguar ameibua mijadala nchini humo baada ya kuwasilisha hoja kuwa umri wa kustaafu upunguzwe.
Jaguar amependekeza umri wa kustaafu upungue kutoka miaka 60 hadi 50 ili kuongeza ajira kwa vijana.
Akitoa mapendekezo hayo leo Septemba 12, 2019, Jaguar amesema kuwa Kenya inakabiliwa na uhaba wa ajira kwa asilimia 55, Na wahanga wakubwa ni vijana.
Kwa mujibu wa takwimu alizozitoa, Amesema vijana 800,000 wanaingia kwenye soko la ajira nchini Kenya lakini wanaopata nafasi ni vijana 70,000.
Endapo mabadiliko hayo yatafanikiwa, Nafasi 25,000 zinazotumikiwa na watumishi wa umma wenye umri kati ya 50-60, zitakuwa wazi.
Tamko hilo, Limeungwa mkono na vijana wengi kwenye mitandao ya kijamii nchini Kenya wakidai kuwa litapunguza tatizo la ajira.
Hata hivyo, Tamko hilo huenda lisipite kwa urahisi kwani watu wenye umri mkubwa nchini humo, Wamekuwa wakileta pingamizi.
The total Public Service workforce is one million. This includes government ministries and parastatals, the Teachers Service Commission (TSC), county governments and those in the disciplined forces..
— Hon. Jaguar (@RealJaguarKenya) September 12, 2019
Should the government review retirement age fron 60 to 50 years, 100,00 out of 800,000 college and university graduate youths would get acess into the job market..
— Hon. Jaguar (@RealJaguarKenya) September 12, 2019
Kenya’s total unemployment rate stands at 26.4 % among the economically active population of 22 million Kenyans. More worrying is that a staggering 85% of the economically active persons who are unemployed are youth.
— Hon. Jaguar (@RealJaguarKenya) September 12, 2019
Miezi miwili iliyopita, Jaguar alishambuliwa mtandaoni kwa kutoa kauli ya kibaguzi, Jambo ambalo lilimfanya awaombe radhi wafanyabiashara wa kigeni nchini humo.
Soma zaidi – http://bongo5.com/mbunge-jaguar-akamatwa-na-polisi-kenya-kwa-uchochezi-na-ubaguzi-video-06-2019/