Je! Unaifahamu familia ya Jose Chameleone?
Chameleone ni baba anayeipenda familia yake na anayewajibika kuiweka katika mazingira mazuri kadri awezavyo.
Chameleone ana watato wanne. Mtoto wa kwanza ambaye ni wa kike anaitwa Ayla Mayanja Onsea aliyemzaa kwenye mahusiano yake na Dorotia. Leo (September 18, 2012) msanii huyo kupitia ukurasa wake Facebook, ameweka picha ya Ayla anayeonekana kukua, huku akiandika ‘Guess’.
Katika ndoa yake na Daniella, Chameleone ana watato watatu. Abba Marcas Mayanja akiwa wa kwanza kwenye ndoa yao, Alfa Mayanja mtoto wao wa pili na
Alba Shyne Mayanja aliyezaliwa February mwaka huu.
September 3 mwaka huu, himaker huyo wa Valu Valu, aliamua kuvishambulia vyombo vya habari vya nchini Uganda kwa kuandika habari za uongo juu ya familia yake, “it’s a pity how media is telling lies for money!! I am clearing the air,my beautiful wife, Abba, Alfa and Alba are not in Mutungo as alleged by media, my family is on holiday in Italy, and not bothered by the rubbish haters are trashing! Please respect peoples families, my family please enjoy your holiday!!!! No stress!”
Hivyo pamoja na kuonekana kama ni mzee wa shari, mashabiki wanatakiwa kujua kuwa Chameleone ‘is a responsible father’.