Habari
Je! Wajua Deddy wa B’Hits ni mtoto wa Juma Kakere hitmaker wa Betty na Safari?
Huenda ukawa mmoja wa watu wengi ambao walikuwa hawafahamu kuwa muimbaji mkongwe wa nyimbo za dance nchini, Juma Kakere ana mtoto aliyeamua kufuata nyazo za baba yake. Mtoto huyo ni Fareed Juma Kakere aka Deddy.
Juma Kakere anafahamika kwa hits zake, Betty na Safari..
Deddy si mpya kwenye ramani ya muziki wa Tanzania. Ni member wa kundi la Unknown lenye wasanii watatu akiwemo Godzilla na Gosby.Amewahi kushirikishwa na Mabeste kwenye ngoma yake, Dole na hivi karibuni ataonekana kwenye video ya Feza Kessy, Amani ya Moyo.
Deddy ni msanii wa reggae/dancehall na ukimsikiliza kwa mara ya kwanza unaweza kuhisi ni mjamaica.