Burudani

Jerry Muro aiandikia barua TFF ya kuomba kupunguziwa adhabu

Hatimaye msemaji wa Yanga Jerry Muro ameinua mikono juu na kuiangukia TFF kwa kuandika barua ya kuomba kupunguziwa adhabu ya kufungiwa kutojihusisha na masuala ya soka kwa muda wa mwaka mmoja.

Adhabu ya Muro ilianza Julai 7, 2016 hiyo inamaanisha tayari ameshatumikia adhabu yake kwa kipindi kisichopungua miezi sita.

TFF kupitia kamati ya maadili ilimfungia Jerry Muro kutokana na kutumia maneno ambayo si ya kiungwana michezoni hususan soka.

Source: Shaffih Dauda

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents