Habari

Jerusalem : Kituo kipya cha treni kupewa jina la Donald Trump

Waziri wa uchukuzi nchini Israel,Yisrael Katz ametaka kuchimbwa kwa reli ya chini kwa chini kwenye mji wa zamani wa Jerusalem karibu na ukuta wa Magharibi na kupewa jina la Donald Trump.

Yisrael Katz alisema kuwa anataka kumpa heshima Rais huyo wa Marekani kufuatia uamuzi wake wa kutambua Jerusalem kuwa mji mkuu wa Israel.

Reli hiyo mpya ya chini na kituo cha treni ni sehemu ya mradi wa reli ya mwendo kasi kutoka Tel Aviv inatarajiwa kuzinduliwa mwaka ujao.

Bw. Katz aliliambia gazeti moja la Israel la Yedioth Ahronoth kuwa kuongezwa kwa reli kutoka Tel Aviv kwenda Jerusalem ndio mradi muhimu zaidi kwa wizara ya uchukuzi.

Chanzo: BBC

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents