Habari
Kamanda wa polisi mkoa wa Singida afariki dunia
Aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa Singida, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Peter Kakamba amefariki dunia leo alfajiri katika hospitali ya Taifa Muhimbili alipokuwa akipatiwa matibabu.
Mwili wa Marehemu utaagwa leo saa 11: 00 jioni katika hiyo na baadaye kusafirishwa kwenda Singida kwaajili ya kuagwa tena na baadaye kwenda nyumbani kwao Rukwa kwaajili ya mazishi.
Kamanda Kakamba alikuwa amelazwa hospitalini hapo akisumbuliwa na maradhi ya tumbo na alikuwa amefanyiwa oparesheni hivi karibuni.
BY: EMMY MWAIPOPO