Habari

Kesi ya Mhe. Mbowe na Ester Matiko yapigwa kalenda

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, imeahirisha kesi inayowakabili viongozi wa CHADEMA, hadi Disemba 21 kwaajili ya kutajwa wakati ikisubiri uamuzi wa Mahakama ya Rufaa iliyokatwa na upande wa mashtaka kupinga usikilizwaji wa rufaa ya Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe na Mbunge wa Ester Matiko.

Aidha Hakimu Mkazi Mkuu wa mahakama hiyo, Wilbard Mashauri ameridhia taarifa ya kutofika mahakama kwa Mbunge wa Kawe, Halima Mdee na Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche ambao wako nchini Burundi wakishiriki michuano ya mabunge ya Afrika Mashariki.

Hakimu mkazi huyo na upande wa mashtaka wamesema hawana pingamizi juu ya uwepo wa taarifa za uzuru huo kutokana na kupokea nakala za barua za ruhusa kutokana Bungeni.

Related Articles

Back to top button

Adblock Detected

Please don't block our ads, we rely on these ads to serve you with credible contents